Salome ni filamu ambayo nimeitunga kutokana na nyimbo yangu ya Salome. Ila filamu hii bado ipo kwenye maandishi na haijachezwa. Kwa sasa tunatafuta mfadhili ili aweze kuwekeza katika filamu hii ili iweze kuchezwa kwa vitendo.

 

Kama umevutiwa na story na unapenda kunisapoti bonyeza hapo na tafuta mawasiliano na mimi.

 

Hapo chini unasoma story ya Salome:

 

 

 

SALOME

 

 

FILM 2012

 


 

 

SALOME

Wasifu wake

§  Awe msichana mwenye umri wa miaka 16

§  Awe na rangi ya maji ya kunde

§  Umbo sio mnene wala sio mwembamba

§  Asiwe mrefu wala mfupi, mpole, mcheshi. Ni mwanafunzi wa shule ya msingi darasa la saba anapenda sana kusoma na kushirikiana na wenzake katika mambo mbalimbali.


 

MAMA SALOME

Wasifu wake

§  Awe mtu mzima mwenye umri wa miaka 35

§  Rangi ya maji ya kunde

§  Asiwe mrefu wala mfupi

§  Awe mnene kiasi

§  Anapenda kazi za nyumbani na kusuka ukili

§  Mcheshi mwenye maneno mengi

§  Anapenda utamaduni

  

 

BABA SALOME

Wasifu wake

§  Awe mtu mzima mwenye umri wa miaka 37

§  Mrefu kiasi na mwembamba kiasi

§  Mweusi kidogo

§  Awe mkali anachokiongea

§  Anapenda kifanyiwe kazi

§  Anapenda kukaa nyumbani


 

BABU SALOME

Wasifu wake

§  Awe mwenye miaka 60

§  Mrefu kiasi na mwembamba kiasi

§  Mweusi kidogo

§  Awe mcheshi anapenda matani

§  Anapenda sana utamaduni

§  Anapenda kukaa na panga muda wote

 

  

BIBI SALOME

Wasifu wake

§  Awe mwenye umri wa miaka 54 hadi 57

§  Mfupi kiasi

§  Rangi yake ni maji ya kunde

§  Awe mpenda kukubali kila jambo

§  Awe anayependa kutembea peku

§  Anapenda kulima

§  Awe mwembamba kidogo

 

 


 

 

 

 

SINI: 1

 

Salome anaonekana darasani akiwa na wenzake huku mwalimu akiwa ana fundisha na Salome akionekana akiwa mwepesi wa kujibu maswali ya somo la Kiswahili.

 

MWALIMU

Mwalimu anandika ubaoni kisha anawageukia wanafunzi na kuwauliza maswali.

Mgaagaa na upwa?

 

SALOME

Anasimama na kujibu swali.

Hali wali mkavu.  

 

MWALIMU

Anaonekana akimsifia Salome alivyojibu vizuri.

Safi sana Salome mpigieni makofi.

 

WANAFUNZI WOTE

Wakipiga makofi wengine wakipiga juu ya dawati.

 

MWALIMU

Mwalimu anaoneka akiwapa maelezo wanafunzi kuhusu mtihani wa kumaliza       darasa la saba akiwapa moyo wanafunzi kuhusu swala lakujisomea wakiwa nyumbani.

 

 

 

KATI KUBWA

Wanafunzi wanaonekana wakitawanyika kuelekea majumba. Salome anaonekana   akikimbia nyumbani kwao.

 

 

 

 

SINI: 2

 

NYUMBANI KWA KINA SALOME (MCHANA)

Mama Salome anapepea moto wa kuni. Sufuria ya mihogo ikiwa juu ya majifya. Baba Salome akiwa kakaa uwanjani kwenye kiti mara anamuita Mama Salome.

 

BABA SALOME

Akimuangalia usoni na tabasamu.

Unajua nini, Mama Salome kesho jumamaosi Salome haendi shule, uwahi kumwamsha mapema ili awahi shamba.

 

MAMA SALOME

Akimwangalia Baba Salome kwa uwoga na mshangao.

Lakini kesho wanaendaga kwajili ya mtihani wa kila wiki na hata hivyo uwa haendi bila 200 ili afanye mtihani wa wiki inaweza ikamsaidia siku ya mtihani wa mwisho.

 

BABA   SALOME

Akimwangalia kwa hasira

Sina hiyo hela na nimesema kesho aende shamba. 

 

MAMA   SALOME

Akiwa na uwoga.

Lakini mume wa…

 

BABA SALOME

Naomba ukaendelee na kazi.

 

MAMA SALOME

Mama Salome ananyanyuka na kuelekea jikoni.

 

 

SINI: 3

 

Asubuhi

Salome na mama yake wakiwa shambani wanalima mara Mama Salome anaacha jembe na kukaa chini.

 

SALOME

Akimfuata Mama yake akiwa kashika jembe na kukaa chini.

Vipi? Mama?

 

MAMA SALOME

Akiguna huku akimwangalia Salome

Mmh! Nimechoka tu.

 

SALOME

Akitabasamu

Basi tuondoke.

 

MAMA SALOME

Anachukua jembe lake.

Haya twende, maana ninavyo jisikia.

 

WOTE

Mama Salome na Salome wanaonekana wakiweka jembe begani na kuondoka. Wakiwa njiani Salome anamsimulia mama yake mitihani ya shuleni kwao inayotolewa.

 

SALOME

Mama tumebakisha miezi mitatu tufanye mitihani ya kumaliza elimu ya msingi.

 

MAMA SALOME

Sawa lakini umejiandaa vizuri na mtihani?

 

 

SALOME

Akishusha jembe begani na kulishika mkononi, huku akimwangalia mama yake.

Sina uhakiaka sababu mtihani ule wakujipima nilikuwa mtu wa pili kati ya watoto thelathini.

 

MAMA SALOME

Akimwangalia Salome.

Sawa umesema mtihani uliopita, lakini huu kila mtu anakuwa anajiandaa sana.

 

SALOME

Akimwangalia kwa kuhuzunika mama yake.

Mama niamini!

 

MAMA SALOME

Haya, na kusisitiza tu kwa sababu uliniambia unataka kuwa daktari.

 

WOTE

Wanaangaliana na kucheka.

 

 

KATI   KUBWA

Wasichana watatu rafiki zake Salome wakiwa kisimani wanafua.

 

 

RAFIKI NO: 1 MARIAMU

Akimuomba Jeni sabuni akinyoosha mkono.

Jeni, niazime sabuni yako kidogo yangu imeisha.

 

JENI

Akibinua mdomo kwa dharau.

Ehe, mwenzangu mama kaniambia nisiimalize. Siwezi kukupa!

 

 

 

MARIAMU

Akiachia mdomo kwa mshangao.

Kwani nimekuambia namaliza si kidogo tu.

 

JENI

Akiendelea kufikicha nguo iliyokuwa kwenye ndoo.

Kwa kifupi sitaki wewe umezoea kumuomba Salome leo sasa hayupo na mimi sitaki.

 

RAFIKI NO: 3 HAPPY

Akibinua mdomo na kuguna.

Jeni tabia mbaya kwani mama yako atajua. Loo!

 

JENI

Akimwangalia Happy.

Haya, kuhusu wewe simpe.

 

HAPPY

Akichukua sabuni yake.

Ndio nampa.

Akimpa sabuni Mariamu.

 

MALIAMU

Akipokea huku, akitasamu.

Asante Happy. Lakini Jeni utakuwa na shida tu! Tutaonana.

 

JENI

Akiinuka akashika nguo na kwenda kuwanika.

Kwani sasa hivi sikuoni?

 

 

 

 

 

 

SINI : 4

 

USIKU

Salome anaonekana kakaa chumbani kwake kitandani akijisomea huku kibatari kikiwaka baada ya muda anazima kibatari anaamua kulala huku akijifunika kanga.

 

 

 

SINI:5

ASUBUHI: SHULENI

 

Wanafunzi wote wapo darasani pamoja na Salome. Wanafunzi wengine wanajisomea. Salome na rafiki zake watatu wanaongea kuhusu mtihani. Mara mwalimu anaingia   darasani na kunyamazisha kelele. Mara anamuita Salome atoke mbele ya darasa.

 

MWALIMU

Hivi wewe Salome baada ya kusoma umekaa unawasimulia wenzio. Sijui stori gani hivi una akili wewe.

 

SALOME

Akimwangalia mwalimu usoni.

Hapana mwalimu nilikuwa naongea kuhusu mtihani wa taifa ili tujiandae sana.

 

MWALIMU

Akimtolea macho Salome na kukunja sura.

Muongo mkubwa kwanza, angalia hizo uniform zako zilivyo chanika!

 

SALOME

Akijiangalia.

Lakini mwalimu…

 

 

MWALIMU

Akiongea kwa sauti yenye hasira.

Kelele! Sasa uwende kwenu mpaka uje na uniform mpya.

 

SALOME

Kwa huzuni anatoka nje huku akiwaangalia wanafunzi wenzake.

 

WANAFUNZI

Wengine wakimwangalia Salome kwa huruma na wengine wanaendelea kusoma madaftari yao.

 

 

KATI KUBWA

Salome anaonekana amekaa na wazazi wake mbele ya nyumba yao (uwanjani). Baba   akiwa kakaa kwenye kiti huku akishika fimbo. Na Salome na mama yake wamekaa kwenye mkeka. Salome anawaambia wazazi wake kilichomfanya arudi nyumbani mapema.

 

 

MAMA SALOME

Akimwangalia baba Salome usoni.

Kwani sisi masikini tukiwa hatuna hela ya kununua uniform ina maana mtoto hasomi? Basi makubwa!

 

BABA SALOME

Akipigisha chini fimbo yake huku akoingea.

Hivi nyinyi hamjui maskini ni maskini. Akipata bahati kidogo vikwazo vingi vitatokea sasa yote ya nini?

 

MAMA SALOME

Akiguna kwa mshangaoa.

Unamaanisha nini kusema hivyo?

 

 

BABA   SALOME

Akimwangalia Salome.

We Salome hebu nenda kabadillishe nguo, ukae tu. Ikifika siku ya kuolewa uwolewe hakuna kingine.

 

MAMA SALOME

Akimtolea macho baba Salome.

Sasa hayo ndio maneno gani? Badala ya kuwaza tufanyaje ili mtoto aendelee na shule.

 

BABA SALOME

Akinyanyuka na kuelekea shambani.

Waza wewe utatafanyaje. Mimi naenda shamba kuangalia ndege.

 

MAMA SALOME

Akiguna na kunyanyuka kuelekea ndani.

Makubwa basi!

 

 

 

 

SINI:6

 

Wavulana (4) wa kijiji wapo kijiweni wamekaa kwenye gogo wakiwa wamezunguukwa na miti wakijadili kwenda kuiba shambani.

 

Mvulana mmoja: JUMA

Anasimama kisha anaongea.

Sikilizeni kwanza inabidi tujadili shamba gani tunaenda.

 

Mvulana wa pili: OTHU

Akimwangalia Juma usoni.

Mashamba yapo mengi tuchague! Sio kitu cha kujadili!

 

 

Mvulana wa tatu: RAMSO

Kwanza leo tuende shamba la yule mama Salome.

 

Mvulana wa nne: JOSE

Akishtuka na kutoa macho.

Mmenikumbusha, mna muonaje yule mtoto Salome?

 

OTHU

Akimwangalia Jose kwa mshangao.

Kafanya nini?

 

JOSE

Mimi namtaka tusaidiane kumpata, halafu kama kawaida tunashilikiana.

 

RAMSO

Akiongea kwa dharau.

Acheni kujipa tabu yule, tunamkamata tunambaka!

 

OTHU

Akimwangalia Ramso kwa furaha.

Halafu nimekumbuka wale wanakuwaga Salome na wenzake.

 

JOSE

Akiinuka na kuongea.

Twendeni kwenye hilo shamba! Kuhusu Salome na rafiki zake tunamkamata mmoja mmoja, tunambaka! Hakuna kumbembeleza! Sisi ndio watoto wa kijijini!

 

JUMA

Anainuka huku anacheka.

Hilo ndio la maana Jose! Twendeni shamba, mimi njaa inauma kuhusu hao watoto tutawakamata tu mmoja mmoja.

 

 

SINI: 7

MCHANA SAA 8

 

Salome akiwa na marafiki zake watatu Mariamu, Happy na Jane wanaruka kamba uwanjani mbali kidogo na nyumbani kwao. Mara Othu, Ramso, Juma, Jose wanapita wanawaona wakina Salome wanacheza kamba. Salome anarusha yeye na Jeni. Mariamu anaruka. Mara Ramso na rafiki zake wanafika karibu na wakina Salome.

 

JUMA

Akiongea kwa ukali!

We Mariamu hebu njoo mwenyewe!

 

RAMSO

Akiongea kwa dharau.

Hakuna kumbembeleza mtu!

 

SALOME

Anaachia kamba na kumwangalia Ramso.

Hivi nyinyi kwanini hamna ustaarabu?

 

JOSE

Akimnyoshea kidole cha shahada.

Tena wewe nyamaza zamu yako bado.

 

SALOME

Akishangaa na kukunja sura.

Zamu ya nini?

 

JENI

Akishanga na kukunja kamba.

Jamani si mnawajua hao walivyo wakorofi. Bora tuondoke maana wana sifa kama nguru.

 

RAMSO

Akicheka kwa dharau huku akiwaangalia.

Eti mwondoke! Haondoki mtu. Leo ndo leo!

 

 

KATI KUBWA

Salome na wenzake wanaonekana wakikimbia huku. Wakina Ramso wanawakimbiza. Mara Salome anapotezana na wenzake. Salome anakimbilia porini. Anapogeuka nyuma anawaona Ramso na wenzake wanakuja. Anaamua kukimbilia nyuma ya mti mkubwa kwa kujificha.

Ramso na wenzake wanasimama kwenye huo mti aliojificha Salome. Salome anatetemeka kwa uwoga na kuamua kutokambio. Ramso na wenzake wanasikia kishindo cha Salome. Anapokimbia na kufika mbali kidogo anachoka sana. Mara anapumzika na anakamatwa na wakina Ramso.

 

JUMA

Anaongea huku akihema akiwa na hasira macho kayatoa.

Yaani wewe unaweza vipi kutusumbua sisi?

 

SALOME

Akiwa na uwoga huku akihema.

Kwani nimewafanyia nini na mnataka nini kwangu?

 

RAMSO

Akimwangalia Juma na Othu.

Jamani mshikeni! Nianze mimi.

Juma na Othu wanamshika Salome.

 

SALOME

Akitoa macho kwa mshangao huku akitetemeka na machozi yakimtoka.

Jamani ndio mnataka kunibaka nioneeni huruma mnanipotezea ndoto zangu za baadaye!

Akilia.

 

RAMSO

Anaongea kwa dharau huku akimwangalia Salome.

Ahaha! Na mimi hii ndio ndoto yangu!

 

Mara wababa wazima wanatokea wakiwa wamebeba kuni. Ramso na wenzake wanakimbia wakiwa hawajambaka Salome anainuliwa na wale wababa wanampeleka kwao. Salome huku akibubujikwa na machozi kwa uchungu.

 

 

KATI KUBWA

Wale wababa na Salome wanaonekana kwa kina Salome. Wamekaa chini na mama Salome na baba Salome. Salome anahadithia yaliomkuta mpaka kuletwa na wale wababa.

 

 

MAMA SALOME

Akishangaa kwa kelele huku akinyanyuka.

Ehe!, ehe!, ehe! Sikubali hata kama bado hawajambaka mwanangu kuwaachia hawa vijana watazoea. Nimesema sikubali!

 

SALOME

Anaonekana akibubujika machozi huku akiinamia chini.

 

BABA SALOME

Anaonekana akinyanyuka na kuongea huku anaondoka na kuelekea kwa kina Ramso.

Sasa wamechokoza moto wao siwanajifanya hawasikii hapa kijijini leowataniona.

 

WABABA 2

Wana nyanyuka na kumuaga Salome na mama yake.

Sisi tunaenda. Pole Salome.

 

SALOME

Akiwaangalia huku akilia kisha anaitikia na kichwa.

 

WABABA 2

Wananyanyua kuni zao na kumwangalia mama Salome.

Mama Salome, tuweni waangalifu na hawa vijana. Sisi tunaenda.

 

MAMA SALOME

Akimuinua Salome huku akiongea.

Haya karibuni, lakini lazima niwafundishe adabu…

 

 

 

 

SINI: 8

SIKU NYINGINE

 

Baba Salome na mama Salome na wazazi wa Ramso wanaonekana wakikaa kwa kina Ramso wamekaa kwenye mkeka wakiongea.

 

BABA SALOME

Akiongea kwa hasira.

Najua mnajua kitendo alichokifanya mwanenu.

 

MAMA RAMSO

Akishusha pumzi na kuongea.

Ndio jana tumesikia hata sisi tumesikitika na hata hivyo Ramso na wenzake. Mpaka leo hawaonekani.

 

MAMA SALOME

Akiongea kwa hasira huku akimwangalia mama Ramso.

Nyinyi mmepanga kuwatorosha. Lakini sawa!

 

 

 

 

MAMA   SALOME

Akiongea kwa uzuni.

Sio hivyo mama Salome. Mimi na wewe tuna uchungu kama wanawake. Na kama mtoto angekuwa nguo ningegawa.

 

BABA RAMSO

Kweli Ramso angekuwa nguo tungekuwa hatunaye zamani.

 

MAMA RAMSO

Sisi tunachoomba mtusamee sisi. Na hata kama tukimuona tutamkamata kama sio yeye yoyote kati yao tutampeleka serikali ya kijiji. Tena sisi tupo pamoja na nyinyi.

 

BABA SALOME

Ananyanyuka na kumshika mkono mke wake.

Mke wangu, tuondoke.

 

 

 

 

 

SINI: 9

JIONI

 

Ramso na wenzake wanaonekana wakijadiliana wakiwa kichakani.

 

JUMA

Akiwangalia Othu pamoja na Ramso.

Jamani sasa itakuwaje?

 

OTHU

Kakaa chini kajinamia huku akivunjavunja vijiti.

Yaani mimi mwenyewe sielewi.

 

RAMSO

Akiongea huku kasimama.

Sio swala la kujadiliana kilichobaki ni kwenda kijiji kingine kwenda kuanza maisha mapya.

 

OTHU

Anainuka chini huku akijikung’uta majani.

Hilo wazo zuri maana…

 

WOTE

Wanaonekana wanaondoka. Gafla wanakutana na baba Salome. Wanajificha kwenye mti. Baba Salome anapita katika mti huo akiwa amebeba jembe begani. Anaelekea nyumbani kwake. Ramso na wenzake wanatoka mbio wakiwa wanarukaruka mashamba ya watu.

 

 

 

 

 

SINI: 10

 

Salome na wenzake Jeni na Mariamu wakiwa kisimani wanateka maji huku wakiwa wanajadili vitendo vya kina Ramso.

 

JENI

Akinyanyua ndoo akiweka pembeni huku akiwa anaongea.

Afadhali walivyokukosa maana wangekufanyia kitendo cha aibu…

 

SALOME

Akiweka kata kwenye ndoo yake.

Jamani acheni mungu aitwe mungu. Siamini kama nimenusurika...

 

 

MARIAMU

Akimwangalia Salome.

Inabidi uamini kama umenusurika na umshukuru mungu kwa kuwaleta wale wababa!

 

JENI

Akimwangalia Mariamu.

Unachoongea Mariamu ni kweli inatakiwa umshukuru sana mungu.

 

SALOME

Akiweka kata chini anasimama na kushika kiuno.

Nyie acheni tu tubebeni ndoo tuondokeni.

 

 

KATI KUBWA

Salome na wenzake wanaonekana wanabeba ndoo wanaondoka. Mara Salome anafika kwao anatua ndoo huku mama yake akipepea moto.

 

 

 

 

SINI: 11

USIKU

 

Salome anaonekana akiwa chumbani kwake. Anawaza hatari iliyotaka kumkuta. Mara mama yake anaingia chumbani kwake.

 

MAMA SALOME

Hivi kibiriti kiko wapi?

 

SALOME

Anastuka na kujifuta machozi.

Kipo… kipo… jikoni.

 

MAMA   SALOME

Akikaa kitandani kwa Salome na kuongea nae akimwangalia usoni.

Ina maana bado tu haujasahau hayo mambo tushayashughulikia. Si unajua watu wenyewe wamekimbia.

 

SALOME

Ndio na jua mama, ila nasikia uchungu kijijini kote wanaadithia habari zangu.

 

MAMA   SALOME

Anamfuta machozi Salome.

Aaah! We waache tu waongee we lala!

Ananyanyuka na kuelekea chumbani kwake.

 

SALOME

Anazima kibatari. Analala na kujifunika kanga.

 

 

 

 

SINI: 12

 

Ramso na wenzake wanaonekana wakiwa wamekaa sehemu huku wanajadiliana.

 

JUMA

Jamani nimepata wazo. Twendeni kwa mganaga. Hali hii mpaka lini?

 

OTHU

Eheeee hilo wazo zuri. Na mimi nimeshachoka kukimbiakimbia.

 

RAMSO

Akimwangalia usoni Juma.

Sasa huko kwa mganga tunaenda kufanya nini?

 

JUMA

Anaonekana akimwangalia Othu usoni na Ramso.

Ina maana nyie hamujui tunaenda kufanya nini kwa mganga.

 

OTHU

Anaonekana nae na shauku ya kutaka kujua.

Ndio hata mimi nimemuunga mkono kuwa wazo lako zuri. Pia hata mimi sijui nitanaenda kufanya nini. Na ni dawa aina gani? Nimesapoti kuona wazo zuri sababu tu nimechoka maisha ya kukimbiakimbia

 

JUMA

Akiwa anaongea kwa kujiamini.

Kwanza kabisa tupate dawa la kuwashaurisha wana kijiji makosa tuliyo yafanya pili tukienda kuiba hawatuoni. Au nyie mnaonaje?

 

OTHU

Kweli jamani tuondokeni tukamtafute huyo mganga!

 

 

SINI: 13

 

Baba Salome anaenda kijiji cha tatu kwenda kusalimia kwa baba yake na mama yake. Wanaonekana wamekaa chini ya muembe wakijidaliana kuhusu Salome akeketwe.

 

BIBI

Akiongea huku akimwangalia baba Salome usoni.

Hivi binti yakoa tafanyiwa lini tohara maana umri unaenda

 

BABA SALOME

Yaani mama hili swala sijui hata litakuwaje?

 

 

 

BABU

Anainuka na kuongea kwa hasira.

Nimesema mwezi wa kumi na mbili nakuja na mama yako kumfanyia mila.

 

BIBI

Anainuka nakuongea kwa hasira.

Heee! Ukaongee na mke wako mwezi wa kumi na mbili ndio hivyo hatutaki aibu! Anaelekea ndani.

 

 

KATI   KUBWA

Baba Salome na babu Salome wanaonekana wanatoka shamba na majembe yakiwa begani. Huku bibi Salome akiwaelekeza wakina Ramso kwa mganga. Mara baba Salome na babu Salome wanashikana kutua majembe kisha baba Salome anachukuwa ndoo na kuelekea kisimani. Anaelekea njia ile ile wanaopita wakina Ramso.

 

 

BABU SALOME

Akiangalia mlango huku akimwita bibi Salome.

Bibi Salome, hebu njoo umuangalie baba Salome.

 

BIBI SALOME

Anatoka nje kwa mshangao.

Kafanyaje!

 

BABU SALOME

Akimnyoshea kidole baba Salome.

Yule mwangalie! Karudi shambani sasa hivi na anaelekea kisimani.

 

BIBI SALOME

Akiachia mdomo kwa mshangao.

He!

Akimwita baba Salome.

We baba Salome…

 

BABA SALOME

Anaonekana akigeuka nyuma.

 

BIBI SALOME

Akiongea kwa sauti ya juu.

Hebu rudi! Kwa nini unajitesa kama hivyo?

 

BABU SALOME

Anaonekana akitandika mkeka na kulala.

 

BABA SALOME

Anaonekana akiweka ndoo chini na kuongea na bibi Salome.

Unasemaje mama?

 

BIBI SALOME

Kesho asubuhi unaondoka acha kujichosha! Hebu nenda kapumzike na baba yako   yupo pale kwenye mkeka.

Kisha anaingia ndani.

 

BABA SALOME

Anaonekana akielekea kwenye mkeka huku akitabasamu na kuongea peke yake.

Kweli uchungu wa mwana ajuwae mazazi.

 

 

 

 

SINI: 15

 

Baba Salome na mama Salome wakiwa wanakula huku Salome akiwa anaongelea kuhusu mtihani wa taifa.

 

 

SALOME

Salome akimwangalia baba yake na mama yake huku akiwa kashika chakula mikononi na kuanza kuongea kwa furaha.

Na wahaidi wazazi wangu ni lazima ni fahulu ili shida zituishe.

 

MAMA SALOME

Akimwangalia Salome.

Aliekuambia ukifaulu shida ndo zinaisha. Yani kusoma ni kutoa ujinga.

 

BABA   SALOME

Baada ya kuzungumza mambo ya maana wakati kesho shamba. Mbona mtoto wa mzee karinga kasomaa lakini bado anakata mkaa?

 

SALOME

Lakini baba…

kwa unyonge.

 

MAMA SALOME

Sio lakini! Lakini jitahidi ufike chuo. Kuna vitu vingi unatakiwa ujiepushe navyo.

 

BABA SALOME

Anaonekana akinawa mikono huku sura inaonekana ajapendezewa na maongezi yale.

 

 

 

 

 

SINI: 16

 

USIKU

Baba Salome na mama Salome wanaonekana wakiwa chumbani wakiwa wanabishana kuhusu Salome kukeketwa.

 

MAMA   SALOME

Akiongea kwa hasira na sauti ya juu.

Nimesema mwanangu hafanyiwi tohara.

 

BABA SALOME

Akiongea kwa hasira.

Humu ndani nani mwanaume na ni nani baba wa Salome?

 

MAMA   SALOME

Hata kama mnataka kuniulia mwanangu.

 

SALOME

Akiwa chumbani kwake tayari kulala. Anasikia mabishano kwa mbali lakini haelewi kinacho endelea anaamua kugeukia upande wa pili wa kitanda na kuendelea kulala.

 

BABA   SALOME

Akiongea sauti ya juu yenye hasira.

Mimi ndio nimeshasema baba na mama nishaongea nao na mila yetu ina sema ivyo   Salome lazima afanyiwe tohara.

 

MAMA SALOME

Lakini baba Salome si unaelewa athali zakukeketwa?

 

BABA   SALOME

Akiongea kwa hasira.

We nyamaza. Nisije kukupiga sasa hivi.

 

 

MAMA SALOME

Akiwa kachukia huku akimwangalia baba Salome.

Unipige kwa lipi kukwambia ukweli ndo unipige eh!

 

 

SINI: 17

ASUBUHI

 

Salome akiwa anaondoka kuelekea shule. Mama Salome anaonekana akimwangalia Salome kwa huruma kwa kitendo anachotaka kufanyiwa huku akiwa anasisitiza kwa kutingisha kichwa.

 

 

KATI KUBWA

Wanaonekana Juma, Ramso na Othu wakiwa kwa mganga. Anaonekana akiwapokea huku akiimba nyimbo zake za mizimu ya kolelo.

 

 

MGANGA

Mganga anaimba huku akiwakaribisha wakina Ramso.

Mnaonekana mna matatizo makubwa sana.

 

RAMSO NA WENZAKE

Wakitetemeka kwa hofu. Wakijibu kwa pamoja.

Ndio mganga tuna matatizo.

 

MGANGA

Akiongea kwa sauti ya juu huku akitoa macho.

Semeni shida yenu!

 

JUMA

Akiongea kwa hofu.

Salome, mganga.

 

MGANGA

Akicheka kwa sauti ya juu kisha anaongea.

Salome… Salome… Salome…

 

 

OTHU

Ndio mganga Salome! Tunatafutwa kwa ajili yake tunataka dawa la kusahau katika kijiji kizima.

 

MGANGA

Poleni sana! Maana kijiji kizima kimepanga kuwafanyia kitu kibaya. Sasa kwanza wekeni hela zenu katika chungu kisha nawapatia dawa ya kuwasaurisha kabisa makosa yenu kwenye kijiji. Pili nataka muniambie nyinyi katika kijiji chenu mnafanya kazi gani na msinifiche na mkinificha dawa itakataa kufanya kazi!

 

JUMA

Akiongea kwa wasiwasi mkubwa.

Mganga sisi kazi yetu kuibaiba mashambani, ndizi, miogo, mahindi kisha tunaenda kuuza.

 

MGANGA

Ehee! Sasa hivi dawa nitayowapa itawasaidia mkienda kuiba hawawaoni kabisa hata mkipita mbele yao.

 

JUMA NA WENZAKE

Wakiwa wenye sura za furaha kupata dawa waliongea pamaoja.

Asante sana mganga.

Huku wanaondoka.

 

MGANGA

Baada ya wakina Juma kuondoka, mganga alianza kucheka na kuona wajinga wakina Ramso huku akiongea na msaidizi wake.

Wale watoto wajinga nimewapa dawa za uwongo. Waache wakakamatwe ili wajifunze.

 

 

 

 

 

SINI: 18

ASUBUHI

 

 

BABA SALOME

Anaonekana kavua shati kapachika begani. Anatoka nje kibarazani kwake kisha anamuita mama Salome akiwa anaosha vyombo.

Mama Salome njoo mara moja chumbani nina maongezi na wewe!

 

MAMA SALOME

Eeh!? Nini tena mume wangu?

Huku ananyanyuka nakuelekea chumbani.

 

BABA   SALOME

Anaonekana akiwa siriasi kupita kawaida.

Mke wangu, naona unanipanda kichwani na nataka leo hii tukubaliane kuhusu Salome   kukeketwa. Mama yangu nitamueleza nini baba pia mila zetu na hata mizimu ya ukoo wetu na isitoshe familia yetu wote wamekeketwa sasa. Tukimuacha Salome sisi tutachekwa na wanakijiji wote najaribu kufikiria kwa kina mke wangu.

 

MAMA   SALOME

Anaonekana akiwa kanyamaza kimya huku akiwa anaguna.

mmh!...

 

BABA   SALOME

Anaonekana akiwa anamwangalia kwa hasira mama Salome.

Sasa unamaanisha nini ukinyamaza kimya?

 

MAMA   SALOME

Akiwa anaongea kwa unyonge.

Baba Salome! Salome mwenyewe leo ndio kaenda kufanya mtihani wa taifa kumaliza darasa la saba. Sisi huku nyumbani tunagombana. We huoni tutasababisha afeli mtihani.

 

BABA SALOME

Akiwa anaonesha ukali wa maneno akipaza sauti.

Sasa uko pamoja na mimi au laa?

 

MAMA   SALOME

Akionekana kususa huku akitoka chumbani kuelekea nje.

Bwana fanya tu unavyojua…

 

 

 

 

 

 

SINI: 19

BAADA YA MIEZI 2

 

Salome na wenzake wanaonekana wakiwa wanaangalia majibu ya mtihani wa taifa. Salome huku akijikuta amefaulu kipaji mjini kisha anaelekea nyumbani akiwa mwenye furaha kuwaeleza wazazi wake.

 

 

 

 

SINI: 20

 

SALOME

Akiwa mwenye furaha anaongea na mama yake.

Mama nimefahulu! Tena shule ya kipaji mjini!

 

 

MAMA SALOME

Akimuuliza kwa unyonge.

Kweli mwanangu hongera!

 

SALOME

Akimwangalia mama yake.

Mama mbona hauna furaha? Unaumwa? Halafu baba yuko wapi nae nimwambie!

 

MAMA SALOME

Akiwa bado mnyonge

Hapana mwanangu niko sawa. Siumwi. Baba yako kaenda kijiji cha pili kwenda kumchukua babu yako na bibi yako watakuja kesho asubuhi. Tena utawaambia wote kwa pamoja.

 

SALOME

He jamani! Baba safari hii hajaniaga dah!

 

 

 

 

 

SINI: 21

 

BABU

Akiwa anawaangalia wote.

Jamani ayawi ayawi sasa yamekuwa! Hebu bibi Salome tueleze umefikia wapi ili Salome awekwe ndani. Maana swala hili limeshafika wakati wake linatakiwa lifanyike haraka.

 

BIBI SALOME

Akiwa anajihami na kuongea huku akionyesha furaha.

Mimi nimeshaongea na Ngariba. Kesho asubui watakuwa wameshafika.

 

 

MAMA SALOME

Akionyesha mwenye hofu.

Sitoamini mpaka mwanangu nione yuko salama ndo kweli nitaona nimekuza!

 

BABA SALOME

Akicheka kwa sauti.

Ahahahaaaa!! Mpaka hapa tumekuza inabidi tukamchukuwe Salome tumuweke ndani.

 

SALOME

Wakati wakifanya majadiliano hayo, Salome alikuwa dirishani kajificha. Anasikiliza wanachoongea.

 

BIBI SALOME

Asije akachoka leo wakati kesho mama mwali unatakiwa apumzike. Twende nikausaidie kuongea na Salome ili akae ndani maana watoto wa siku hizi anaweza akakuchosha bure.

Anainuka na mama Salome huku wanacheka.

 

 

KATI KUBWA

Mama Salome na bibi Salome wanapofika jikoni wanakuta chakula kinaungua na Salome hayupo. Wanaita bila mafanikio. Wanaenda kuwataarifu baba Salome na babu yake Salome kuwaeleza kuwa Salome haonekani. Baba na babu wanashtuka.

 

MAMA SALOME

Akiongea kwa wasiwasi.

Jamani Salome haonekani na kaacha chakula kinaungua.

 

BABU SALOME

Akistuka.

Kwa nini anaondoka na kuacha chakula kinaungua na hiyo tabia gani?

 

 

BABA SALOME

Anaonekana akifikiria kitu huku anaongea.

Jamani Salome! Mbona hajawahi kufanya kitu cha ajabu kama hiki?

 

MAMA SALOME

Anaonekana kama kachanganyikiwa.

Lakini kweli baba Salome, atakuwa kaenda wapi? Kila akitoka lazima aage.

 

BABU SALOME

Basi kama ndo hivyo tusifanye masiala. Inabidi akatafutwe.

 

SALOME

(Nyimbo inasindikiza kilio.)

Anaonekana akikimbia huku akilia na kuelekea porini. Anapofika katikati ya pori anakaa chini na kuanza kulia kwa uchungu huku akiongea.

Mimi sikubali, sirudi nyumbani mpaka wasahau ni bora niepushe uwahi wangu kwa kukaa huku kwa muda.

Akiendelea kulia kwa uchungu.

(Nyimbo ya Salome inasindikiza kilio.)

 

 

KATI KUBWA

Mama Salome, baba Salome, babu Salome, pamoja na bibi Salome wanaulizia kila nyumba za marafiki zake bila ya mafanikio. Wanaonekana kuchanganyikiwa na kuelekea kwenye maeneo mengine kumtafuta.

 

 

MAMA SALOME

Akiwa kachanganyikiwa na kuongea akiwa na uchungu.
Sasa mwanangu atakuwa kaelekea wapi au atakuwakachukuliwa na nani, hajawahi kuondoka bila kuaga.

 

 

 

BIBI SALOME

Akimuangalia mama Salome.
Sasa mwanangu usilalamike twende tukamtafute.


MAMA SALOME

Sasa mama mpaka saa hizi saa kumi na moja hatujamuona.

BABA SALOME

Akiongea kwa jazba kidogo.

Tunaangaika hivi halafu asije. Akawa katoroshwa na mwanaume.

BIBI SALOME

Mmmmh!! Hayo yanawezekana. Watoto wa siku hizi.

 

BABA SALOME

Kuwa nimekumbuka sisumbuki kumtafuta. Haiwezekani mtu aondoke gafla huyu kashaondoka na mwanaume!

 

BABU SALOME

Akimwangalia baba Salome kwa unyonge.

Usiseme hivo sasa huyu mzazi mwenzako si una mvunja nguvu.

 

BABA SALOME

Sio hivo baba.

Wakiendelea kutembea kumtafuta.

 

 

KATI KUBWA

Wakiwa wanaendelea kumtafuta walipofika katikati ya pori wanashtuka.

Wanapoona kichwa cha Salome na chini kuna damu nyingi na wote wanaishiwa na nguvu na mama Salome anazimia.

 

 

 

Itaendelea part two…

 

 

                 Story

               Oliver John

 

 

 

 

CAST

 

1)       Baba Salome

2)     Mama Salome

3)     Babu Salome

4)     Bibi Salome

5)     Salome

6)     Ramso

7)      Baba ramso

8)     Mama ramso

9)     Juma

10)   Jose

11)     Othu

12)   Mganga

13)   Mbaba namba:1

14)   Mbaba namba:2

15)   Maliamu

16)   Happy

17)    Jeni

18)   Mwanafunzi 1

19)   Mwanafunzi 2

20) Wa baba wawili      

 

 

STORY

OLIVER JOHN

 

SCRIPT WRITER

AISHA ATHUMANI

 

SCRIPT EDITING

ERICK GABRIELY

FRANZISKA MUELLER

 

DIRECTOR

_______________________

 

ASSISTANCE DIRECTOR

_________________________________

 

PRODUCED BY

_______________________________

 

MAKE UP      

____________________________________

 

 

 

CASTING DIRCTOR

______________________________